Ads 468x60px

Mar 10, 2025

RAMADHAN KAREEM - PT 3 [Kiswahili]

Assalaamu alaikum,

 

Natumai hamjambo na mnaendelea na ibada za Mwezi Mtukufu. Tunaendelea na risala yetu. 

 

 

 Baada ya Kumshukuru Allah na kumtakia Rehma Mtume Muhammad , hapo juu ni aya ya 10 na 11 ya Sura As-Swaaf kutoka Quran inayozungumzia jihad na ndiyo itakuwa mada yetu.

 

Tunaendelea na mwezi Mtukufu wa Ramadhani, mwezi ambamo mambo kadhaa yamedhihirika. Ni katika mwezi huu saumu ikafaradhishwa, qiyam ya usiku yaani sala ya tarawih ikawekwa ni jambo la thawabu, ni mwezi wa kuomba dua na ni mwezi ambamo dua inakubalika. Pia ni mwezi ambamo mna usiku wa Lailatul Qadri. Fadhila nyingine ni kuwa Quran imetelemshwa katika mwezi huu.

Wafasiri na wanazuoni wakuu wanaelezea kuwa vitabu vyote vya mbinguni vimeteleshwa katika mwezi huu.

 

Ni katika mwezi huu katika maeneo ya Badri, vita kati ya Waislamu na makafiri, iitwayo vita vya Badri, ilitokea ambayo ilidhihirisha ujasiri wa Uislamu. Makafiri walidhalilika mno na hawakutegemea kabisa. Hivyo leo tutazungumzia kuhusu vita vya Badri ili kujipatia thawabu za kuwakumbuka Masahaba mashujaa waliojitolea kwa hali na mali kuitetea Uislamu.

 

Tafsiri ya aya: Enyi mloamini, je Nisiwaonyeshe biashara itakayowaokoa na adhabu kali? Muaminini Allah na Mtume Wake, na piganeni jihad katika njia ya Allah, kwa mali yenu na nafsi zenu, haya ni bora kwenu ikiwa mnafahamu. (SURA: AS-SWAFF: 10-11)

 

Biashara ni jambo ambalo inampatia mtu faida. Hapa Allah Anazungumzia kuleta imani juu ya Allah na Mtume Wake, kusoma kalima, ndipo itamletea mtu faida; vinginevyo hatapata faida yoyote. Kisha Allah akaagiza jihad katika njia Yake kwa mali na nafsi zetu; na hii akaitaja kuwa ni bora kwetu.

 

Hivi sasa Waisalmu wanadhalilika ulimwenguni ni kwa sababu ya kuacha jihad. Pili mali na pesa imewafanya watu kuwa waoga. Tatu jihad huzidisha hadhi ya Uislamu. Uislamu ni dini ya amani, lakini pindi inapoandamwa kutaka kuangamizwa, basi ni vyema ikahifadhiwa kwa jihad. Anaeuawa katika jihad ni shahidi. Pia anaejeruhiwa katika jihad, basi siku ya kiyama damu itatoa ushahidi wa kunukia kama zafarani. Shahidi hataogeshwa bali atakafiniwa katika nguo zenye damu, atasaliwa jeneza na kuzikwa. Siku ya kiyama atafufuliwa na nguo zake za damu.

 

Hadithi: Mtume amesema kuwa mtu mwenye macho aina mbili hataingia motoni. Moja: ni mwenye kutokwa na machozi katika hofu ya Allah na PILI macho yaliyokesha wakati wa jihadi ikichunga uvamizi wa adui.

Hadithi: Mtu huyu hataingia motoni ambae miguu yake ikapatwa na vumbi katika njia ya Allah.

 

 

Katika vita vya Badri, Waislamu walikuwa 313 tu wakiwa na farasi 17 tu na mikuki kama 8 na pia hawakujianadaa kabisa kupigana. Makafiri walikuwa kati ya 900 na 1,000 na kila mmoja alikuwa na farasi au ngamia na vifaa vyote na walijiandaa kikamilifu. Makafiri walikuja na dhamira ya kuwadhalilisha Waislamu. Masahaba walimtayarishia Mtume banda la kukaa na kutoa amri. Iliponadiwa nani atakaemlinda Mtume , AbuBakr Siddiq ndiye aliyejitokeza.

 

Makafiri 70 waliuawa katika vita wakati Masahaba 14 tu wakawa mashahidi. Usiku wa kuamkia siku ya vita, Mtume alipotembelea uwanja wa vita, aliweka alama kuwa kafiri Fulani atakufa hapa na Fulani hapa, na ndivyo ikawa.

 

Wakati wa vita, walikuja watoto wawili kwa AbdulRahman bin Auf na kumwambia waonyeshwe aliko Abu Jahal ili wakamuue kwani anamtukana sana Mtume . Walipoonyeshwa, mmoja alimpiga panga la nguvu hadi mguu kuvunjika. Jeuri lake likawa pale tu kwani kabla ya kufa alisikitika mno kupigwa na watoto wadogo badala ya jemedari kama yeye.

 

Maswali / maoni yanakaribishwa.

 

JazakAllah.

0 comments:

Post a Comment

Enter your Comment here...

 

Visitor's Traces

Total Page views