Ads 468x60px

Jul 30, 2013

RAMADHAN KAREEM - PT 9 (LAYLATUL QADRI)‏ (KISWAHILI)


Assalaamu alaikum,
Natumai hamjambo na mnaendelea na ibada ya swaum pamoja na ibada zingine. Mwezi mtukufu ndyo inatukimbia kwa kasi sana kwani tunakamilisha theluthi 2 yake leo, hivyo bado theluthi tu!!
Baada ya Kumshukuru Allah na kumtakia Rehma Mtume Muhammad Swallallahu Alaihi Wasallam, Sura Qadr inazungumzia fadhila za usiku wa Laylatul Qadri. 
Fadhila za Laylatul Qadr.
Aya: Hakika Tumeitelemsha (Quran) katika usiku uliotukuka (wa Laylatul Qadri). Ewe Mtume Swallallahu Alaihi Wasallam, je unafahamu Laylatul Qadr ni nini? Laylatul Qadr ni bora kuliko ibada ya miezi 1,000. (humo) Malaika hushuka pamoja na Jibrael, kwa idhini ya Mola wao na wanaomba usalama na amani hadi alfajiri inapotanda.
Mtume Swallallahu Alaihi Wasallam alikuwa akiwasimulia Masahaba ujasiri wa Mcha Mungu wa Bani Israel, ambae mchana hufunga saumu na kupigana jihad na usiku hukesha katika ibada ya Allah, ilikuwa hivyo kwa miaka 400; tukumbuke kuwa watu wa umati zilizopita, pamoja na umri zao kuwa mkubwa, hata miili yao ilikuwa kubwa na pana.
Masahaba wakahuzunika na kusema Ewe Mtume Swallallahu Alaihi Wasallam, bila shaka hao watatuzidi katika thawabu kwani sisi umri zetu ni fupi. Allah Akatelemsha sura nzima ya Qadri kuwapa habari njema umma wa Mtume Swallallahu Alaihi Wasallam.
Baadhi ya alama zinazopatikana katika usiku wa Laylatul Qadri ni kuwa usiku huo mbwa hawabweki, maji ya bahari ambayo ni chungu lakini usiku huo huwa tamu kupita asali, nyota za mbinguni hazianguki, kunakuwa na utulivu usiku huo, kama upo ndani ya ibada na ukajihisi mwili kusisimka basi elewa kuwa Malaika mtukufu Jibrael amekupa mkono.
 Ni usiku wa kufanya ibada kadri tuwezavyo, tuombe dua kwa Allah kwani Allah Anafurahi sana kuona waja wake wakimuomba. Mtume Swallallahu Alaihi Wasallam alitoa mfano wake kuwa mtu 1 alisafiri na ngamia wake akiwa na chakula cha kutosha. Alipofika porini, alishtukia ngamia wake ametoweka, hivyo hakuwa na la kufanya. Akalala huku akaweka kichwa juu ya jiwe anasubiri kifo. Alipozinduka, alimuona yule ngamia wake amesimama kichwani mwake. Mtume Swallallahu Alaihi Wasallam akawauliza Masahaba, niambieni huyu mtu atakuwa na furaha kiasi gain? Masahaba wakajibu kuwa furaha isiyo na mfano. Mtume Swallallahu Alaihi Wasallam akasema Allah zaidi kuliko huyo mtu wakati mja anapomuomba.
Pia ni bora kusoma Qasida Burdai kwani ni Qasida iliyokubalika kwa Mtume Swallallahu Alaihi Wasallam na hivyo ina faida tele.
Kithirisha kusoma: ALLAHUMMA QINA ADHABANNAARI WA-ADKHILNAL JANNATA MA-AL ABRAARI YAA AZIZU YAA GHAFFAARI, katika siku 10 za mwisho.
Allah atukubalie ibada zetu, amin.

Maswali / maoni yanakaribishwa.
JazakAllah,
Muhammad KHATRI

Jul 29, 2013

The wealth of this world...

The wealth of this world is nothing compared to the wealth of Love of RasulAllah ﷺ, His Ahlul Bayt & His Companions RadiAllahu Ta'ala Anhum

Aurat Aurat Hai...

Farmane Pyare Mustafa (SwallAllahu Alaihi Wa Sallam):
Aurat Aurat hai, yani Parde me rakhne ki chiz, jab wo baahar nikalti hai to Shaitan use Ghoorta hai.

[Tirmizi Sharif]

Kutte ki paidaish kis tarah hui?


Q.
Kutte ki paidaish kis tarah hui?

A.
Kutte ki paidaish is tarah hui ke ALLAH Paak ne jab Hazrat Adam AlaihisSalaam ka Putla Mubarak tayyar farmaya to Farishte Hazrat Adam AlaihisSalaam ke us putle Mubarak ki Ziyarat karte the, magar Shaitan mardud Hasad ki Aag me jal bhunj gaya-aur ek martaba us mardud ne Bugz-o Keena me aakar Adam AlaihisSalaam ke Putle Mubarak par thook diya-ye thook Hazrat Adam AlaihisSalaam ki Naaf Mubarak ke maqam par padha.
ALLAH pak ne Hazrat Jibreel AlaihisSalaam ko hukm diya ke us jagah se utni mitti nikal kar us mitti ka kutta (DOG) banado-chunanche us shaitani thook se mili hui Mitti ka Kutta bana diya gaya.
Ye kutta Aadmi se maanoos is liye hai ke mitti Hazrat Adam AlaihisSalaam ki hai,aur paleed isliye hai ke Shaitan ka thook mila huwa hai,aur RAAT ko jagta isliye hai Haath use Hazrat jibreel AlaihisSalaam ke lage haiN.

[RUHUL BAYAN,JILD 1,SAFA 86]

Jul 28, 2013

RAMADHAN KAREEM - PT 8 (SWALI / JIBU)‏ (KISWAHILI)


Assalaamu alaikum,

Natumai hamjambo na mnaendelea na ibada ya swaum pamoja na ibada zingine.
Kuna ndugu yetu ameandika maoni yake na kuuliza swali pia, na kama ilivyo ada yangu, huwa simtaji muulizaji. Maoni/ swali ni hii ...

SWALI: Leo nina maoni tu na kama nitakosea naomba unirekebishe Inshaallah nia ni kuipeleka mbele Dini hii tukufu ambayo ndio njia sahihi ya kuiendea Jannah ya Allah. Tumesisitizwa sana kwamba tunapohitilafiana turudi kwenye kitabu kitakatifu Qur an pamoja na Sunna za Mtume wetu Muhammad (SAW). Mimi sijakubaliana na ushauri ulioutoa wa kuwahusia waislam kutokuswali katika misikiti ya Answar Sunnah.
Mimi naamini sisi kama waislam tumesisitizwa sana kwenye suala la umoja(Tushikamane kwenye kamba moja na tusifarakane), na umoja ndio ambao utatuletea maelewano miongoni mwetu na kuwa na mawasiliano mazuri. Je ni vipi utaweza kumuelimisha Yule ambaye unaona anakosea wakati unamkimbia, Je nini hukumu ya Yule anayesikia Adhana kwenye msikiti uliokaribu na kuenda msikiti wa mbali kwa ajili ya sala na baadae kurudi hapo alipo? Kama nilivyotangulia kubainisha mwanzo tumehimizwa njia za kuziendea Khilafu zilizopo, badala ya kumkimbia mtu muelimishe kwa nini anachofikiria au anachokifanya sio sahihi kwa kutumia Aya za Qur an na Hadith za Mtume(SAW).
Hiyo peke yake ni mada tofauti na ina malumbano yasiyoisha!! Answar Sunnah (kwa hapa Afrika Mashariki), wahabi (sehemu nyingi duniani), Ahlul Hadith (sehemu kubwa ya Bara Hindi), Salafi (sehemu kubwa ya Uarabuni) ni baadhi tu ya majina yamebuniwa na vikundi hivyo - wote wakiwa na lengo takriban moja tu. Mwanzilishi mkuu alikuwa Muhammad ibn AbdulWahab wa Najdi (sasa Riyadh) Saudia. Siri zake za jinsi alivyonunuliwa na waingereza ili tu kuleta mfarakano miongoni mwa Waislamu na Usilamu kwa ujumla na hasa kupunguza mapenzi ya Mtume Swallallahu Alaihi Wasallam katika mioyo ya Waislamu, unaweza kuzisoma katika kitabu "Confessions of a British Spy", ambacho nimeambatanisha kwa faida na manufaa yetu sote.
Kwa muhutasari tu, licha ya kusomewa Aya za Quran Tukufu au Hadithi, lakini bado wanashikilia msimamo wao ili kutekeleza matakwa ya vibaraka zao!! Kusali pamoja nao kuna madhara ya kuwa wengine nao watadhani kuwa "huyo nae ni miongoni mwao!!" Ni sawa na kusema mimi nimeingia baa labda kununua soda, ila nitadhaniwa pengine ni "mnywaji"!! Ndyo maana wanazuoni wamesema ni bora kujiepusha.
Vile vile tukumbuke Hadithi ya Mtume : "ummah wangu itagawanyika katika makundi 73, vyote vitakuwa vya motoni isipokuwa moja tu". Hivyo kauli ya Mtume haitakuwa ya uongo abadan!!

Naamini tukianza utengano huu hautishia hapo, kwani tutasema tusiswali kwenye misikiti ya Ibadh, lakini sio hilo tu tusisali na wale wanaofungia sala kifuani, au wanaofungia chini ya kifua au wasiofunga mikono kwenye sala, pia wale wanaotoa salam moja baada ya Shahad ya mwisho na vile vile wale wanaokunut nawale wasiokunuti. Tutaanza utengano misikiti na miskiti lakini haitaishia hapo tutakuja kati ya waumini ndani ya msikiti mmoja(je hatujaona au kusikia misikiti ikiswali jamaa mbili kwa mara moja kutokana na misimamo tofauti?) na mwisho tutaishia kati ya muumini na muumini.

Ikiwa Muislamu anatekeleza / kufuata kanuni ya mmojawapo kati ya Maimamu wanne, basi yumo kwenye njia sahihi.

Kwa uelewa wangu mdogo tofauti zetu kubwa zimekuwa kwenye mambo ya Sunnah tunapoongelea mambo ya fardhi tunakuwa pamoja. Nafikiri cha muhimu kwenu wanazuoni kutuelimisha sisi maamuma na sisi maamuma vile vile kufanya jitihada ya kuijua Dini yetu tukufu kwa njia mbalimbali na kuacha kusema mimi tu nilisikia kwa shehe huyu au shekhe Yule, Allah ametupa akili tufanyie kazi yote yanayotuijia(simaaninishi tusiwasikilze Mashekhe zetu bali tujaribu kupima tunayoyapata kwa akili zetu) maana kila mtu atahukumiwa kivyake. Tuna vita kubwa ya kuhakikisha kwanza kabisa kwenye Umma huu wa uislam tunao ndugu zetu wengi sana ambao hata hawatekelezi nguzo muhimu ya Sala, na hao wanaachwa tunasema shauri zao, tutakuja ulizwa kuhusu hilo. Tunaondugu zetu wengi wanaokubali kuitwa wageni misikitini kila mwaka, maana inapokaribia Ramadhani utasikia jamani tujiandae kuwapokea wageni miskitini na Ramadhani ikiisha wanaondoka, tuwafanyie kazi hawa wabaki misikitini. Hebu tujiulize ndugu zangu uingie nyumbani kwako halafu mwanao amwite mkeo anamuambia mama kuna mgeni amekuja sababu hakuoni nyumbani utajisikiaje, ndugu zangu waislam Misikiti ndio nyumba zetu za ibada tuipambe kwa kuijaza muda wote wa mwaka na sio Ramadhani,Ijumaa na siku ya saal za Eid tu.
NB: Nilikuwepo kwenye hutba moja ya ijumaa Ramadhani ya mwaka jana kwenye msikiti wa Vetenary kwa sheikh Kishki, mada ilikuwa ni ipi idadi kamili rakaa za salat Taraweh(huwa anakuwa na CD anauza lakini wametengeneza kitabu kidogo kutokana na hutba hii,unaweza vitafuata), nilifurahi sababu alijitahidi kuelezea vizuri kuhusu pande hizi mbili na Hadith wanazosimamia. Lakini pamoja na kuonyesha msimamo wake ni upi, ushauri wake ulikuwa kwamba ukiswali kwenye msikiti wanaosali rakaa 20 hakikisha unasali na imamu mpaka mwisho nausikatishe kwa sababu kuna faida kubwa kuanza na kumaliza na imamu na hata ukiswali kwenye msikiti wa naosali rakaa nane hivyo hiyo.

Nimepata kusikia sifa za huyu shekhe, ila sielewi kama alijaribu tu kutowakasirisha wanaosali rakaa 8 au vipi. Ila wanazuoni wanasema mwenye kusali rakaa 8 anaenda kinyume na mafundisho ya Mtume Swallallahu Alaihi Wasallam na baya zaidi anadanganya kwani rakaa 8 ni tahajjud na sio taraweh!!

Samahani kwa kukuchosha kwa maelezo mengi hii inatokana na elimu ndogo, naomba kusahihishwa nilipokosea.

JIBU: Kwanza kabisa naomba nieleweke kuwa mimi si shekhe ila pengine kwa sababu tu napendelea kutoa risala kutokana na mafundisho ninayoyapata, basi wengi hudhani mimi ni shekhe; hivyo kukosea/ kuteleza katika maoni ni jambo la kawaida.
Pia kutokana na urefu wa maoni/ swali, nimejaribu kujibu baada ya paragraph ya swali hapo kwa wino mwekundu.
Natumai nimejaribu kuchambua swali / maoni, ila kama bado kuna dosari basi nitafurahi kuambiwa ili tujaribu kuelimishana.


Maswali / maoni yanakaribishwa.

JazakAllah,
Muhammad KHATRI 

 

Visitor's Traces

Total Page views