Ads 468x60px

Mar 10, 2025

RAMADHAN KAREEM - PT 3 [Kiswahili]

Assalaamu alaikum,

 

Natumai hamjambo na mnaendelea na ibada za Mwezi Mtukufu. Tunaendelea na risala yetu. 

 

 

 Baada ya Kumshukuru Allah na kumtakia Rehma Mtume Muhammad , hapo juu ni aya ya 10 na 11 ya Sura As-Swaaf kutoka Quran inayozungumzia jihad na ndiyo itakuwa mada yetu.

 

Tunaendelea na mwezi Mtukufu wa Ramadhani, mwezi ambamo mambo kadhaa yamedhihirika. Ni katika mwezi huu saumu ikafaradhishwa, qiyam ya usiku yaani sala ya tarawih ikawekwa ni jambo la thawabu, ni mwezi wa kuomba dua na ni mwezi ambamo dua inakubalika. Pia ni mwezi ambamo mna usiku wa Lailatul Qadri. Fadhila nyingine ni kuwa Quran imetelemshwa katika mwezi huu.

Wafasiri na wanazuoni wakuu wanaelezea kuwa vitabu vyote vya mbinguni vimeteleshwa katika mwezi huu.

 

Ni katika mwezi huu katika maeneo ya Badri, vita kati ya Waislamu na makafiri, iitwayo vita vya Badri, ilitokea ambayo ilidhihirisha ujasiri wa Uislamu. Makafiri walidhalilika mno na hawakutegemea kabisa. Hivyo leo tutazungumzia kuhusu vita vya Badri ili kujipatia thawabu za kuwakumbuka Masahaba mashujaa waliojitolea kwa hali na mali kuitetea Uislamu.

 

Tafsiri ya aya: Enyi mloamini, je Nisiwaonyeshe biashara itakayowaokoa na adhabu kali? Muaminini Allah na Mtume Wake, na piganeni jihad katika njia ya Allah, kwa mali yenu na nafsi zenu, haya ni bora kwenu ikiwa mnafahamu. (SURA: AS-SWAFF: 10-11)

 

Biashara ni jambo ambalo inampatia mtu faida. Hapa Allah Anazungumzia kuleta imani juu ya Allah na Mtume Wake, kusoma kalima, ndipo itamletea mtu faida; vinginevyo hatapata faida yoyote. Kisha Allah akaagiza jihad katika njia Yake kwa mali na nafsi zetu; na hii akaitaja kuwa ni bora kwetu.

 

Hivi sasa Waisalmu wanadhalilika ulimwenguni ni kwa sababu ya kuacha jihad. Pili mali na pesa imewafanya watu kuwa waoga. Tatu jihad huzidisha hadhi ya Uislamu. Uislamu ni dini ya amani, lakini pindi inapoandamwa kutaka kuangamizwa, basi ni vyema ikahifadhiwa kwa jihad. Anaeuawa katika jihad ni shahidi. Pia anaejeruhiwa katika jihad, basi siku ya kiyama damu itatoa ushahidi wa kunukia kama zafarani. Shahidi hataogeshwa bali atakafiniwa katika nguo zenye damu, atasaliwa jeneza na kuzikwa. Siku ya kiyama atafufuliwa na nguo zake za damu.

 

Hadithi: Mtume amesema kuwa mtu mwenye macho aina mbili hataingia motoni. Moja: ni mwenye kutokwa na machozi katika hofu ya Allah na PILI macho yaliyokesha wakati wa jihadi ikichunga uvamizi wa adui.

Hadithi: Mtu huyu hataingia motoni ambae miguu yake ikapatwa na vumbi katika njia ya Allah.

 

 

Katika vita vya Badri, Waislamu walikuwa 313 tu wakiwa na farasi 17 tu na mikuki kama 8 na pia hawakujianadaa kabisa kupigana. Makafiri walikuwa kati ya 900 na 1,000 na kila mmoja alikuwa na farasi au ngamia na vifaa vyote na walijiandaa kikamilifu. Makafiri walikuja na dhamira ya kuwadhalilisha Waislamu. Masahaba walimtayarishia Mtume banda la kukaa na kutoa amri. Iliponadiwa nani atakaemlinda Mtume , AbuBakr Siddiq ndiye aliyejitokeza.

 

Makafiri 70 waliuawa katika vita wakati Masahaba 14 tu wakawa mashahidi. Usiku wa kuamkia siku ya vita, Mtume alipotembelea uwanja wa vita, aliweka alama kuwa kafiri Fulani atakufa hapa na Fulani hapa, na ndivyo ikawa.

 

Wakati wa vita, walikuja watoto wawili kwa AbdulRahman bin Auf na kumwambia waonyeshwe aliko Abu Jahal ili wakamuue kwani anamtukana sana Mtume . Walipoonyeshwa, mmoja alimpiga panga la nguvu hadi mguu kuvunjika. Jeuri lake likawa pale tu kwani kabla ya kufa alisikitika mno kupigwa na watoto wadogo badala ya jemedari kama yeye.

 

Maswali / maoni yanakaribishwa.

 

JazakAllah.

Mar 4, 2025

RAMADHAN KAREEM - PT 2 [Kiswahili]

Assalaamu alaikum,

 

Natumai hamjambo na mnaendelea na ibada za Mwezi Mtukufu. Tunaendelea na risala yetu.

Baada ya Kumshukuru Allah na kumtakia Rehma Mtume Muhammad , imesomwa aya ya Quran inayozungumzia saumu na ndiyo itakuwa mada yetu.

 

Tafsiri ya aya:

Enyi mloamini mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa wale walikutangulieni, ili mpate kumcha Mwenyezi Mungu.

Hadithi tuliyosimulia Ijumaa iliyopita, ina maelezo zaidi, na tutazichambua kwa ufupi.

 

Tumefaradhishiwa saumu. Ila kama kuna mgonjwa au msafiri au mwanamke katika siku za hedhi zake, hao wameruhusiwa kutofunga siku hizo. Baada ya kukamilisha idadi ya 29 au 30, basi wanatakiwa wafunge siku walizoacha. Ila hawaruhusiwi kula hadharani. Pia mtu mzee asiye na nguvu na wala hatarajii kupona, itambidi atoe fidia badala ya saumu zake. Lau kama atapata nguvu, basi ni bora kwake kufunga na si kutoa fidia.

 

Qiyam / ibada ya usiku imefanywa kuwa ni ya thawabu. Ibada ya usiku ni raka 20 za Tarawih, nayo ni Sunnah iliyosisitizwa kwa wanaume na wanawake. Ni bora kwa kina mama kusali nyumbani. Hadi mwanzoni mwa Ukhalifa wa Sayyidina Umar, Masahaba walisali Tarawih peke yao. Ndipo Sayyidina Umar aliwakusanya nyuma ya imam mmoja nae ni Ubay bin Ka'ab, ambae aliwasalisha rakaa 20. Baadhi ya watu wanadai Tarawih ni raka 8. Ikumbukwe raka 8 ni tahajjud na si Tarawih.

Pia kiakili naomba tuzingatie; ikiwa Tarawih ni rakaa 8 na sisi tunasali rakaa 20, siku ya Kiyama Allah Akituuliza kwa nini umezidisha rakaa 12, basi japo tutaweza kumuomba kwa Rehema zake atujaalie thawabu ya ziada kwa hizo rakaa 12. Lakini je wanaosali rakaa 8 na Allah akiwauliza kuwa Tarawih ni 20 kwa nini mkasali 8 tu, hebu jiulize hizo rakaa 12 watazitoa wapi!! Naomba tusipumbazike na wanaodai kuwa eti ni rakaa 8 tu!! Laa hasha! Tarawih ni rakaa 20.

 

Mna usiku mmoja ambayo ibada yake ni bora kuliko ibada ya miezi 1,000. Miezi 1,000 ni miaka 83 na ieleweke kuwa umri wa ummah huu ni karibia miaka 60.

 

Imeelezwa kuwapunguzia mzigo wafanyakazi wenu mwezi huu. Mtume amesema kuwa mwenye kumpunguzia mzigo mfanyakazi wake, basi Allah atampunguzia mzigo siku ya Qiyama.

 

Mtume ameeleza kuwa siku zake 10 za mwanzo Allah anawarehemu waja wake, 10 za kati Allah anawasamehe waja wake na 10 za mwisho ni kuongoka na moto wa jahannam.

Imeelezwa kukithirisha mambo manne: Kalima, istighfar, kuomba Pepo na kuomba huru na moto wa jahannam.

Mwenye kumfuturisha Muislamu mwenzake, hujaaliwa thawabu ya saumu moja mwenye kumnywesha maji, basi Allah atamjaalia maji ya Kauthar na hatashikwa na kiuu hadi kuingia Peponi.

 

Maswali / maoni yanakaribishwa.

 

JazakAllah.

 

Visitor's Traces

1,293 Pageviews
Mar. 12th - Apr. 12th

Total Page views

767162