Ads 468x60px

Jan 30, 2025

SHA'ABAAN [Kiswahili]

Assalaamu alaikum,

 

Natumai hamjambo.

 

Mwezi wa nane katika Kalenda ya Kiislamu ni Sha'abaan. Utukufu wa mwezi huo juu ya miezi mingine ni kama ule wa Mtume juu ya Mitume wengine.

 

BAADHI YA TAREHE MUHIMU:

 

Qiblah ilibadilishwa kutoka Baytul Maqdis na kuwa Al Kaaba.

 

Imam Abu Hanifa, mmoja kati ya Maimamu wanne, kuiaga dunia hii tarehe 2.

 

Imam Husein RadwiyAllahu kuzaliwa tarehe 6.

 

Usiku wa kuwa huru na moto wa Jahannam (au kasimatu rizki) tarehe 15.

 

KUBADILIKA KWA QIBLAH:

 

Baytul Maqdis (Msikiti wa Aqsa) ulikuwa ndiyo Qiblah ya mwanzo ya Waislamu. Karibu Mitume wote waluielekea katika sala zao. Mtume alitamani sana kuelekea Al Kaaba tangu mwanzo tu.

 

Kila Mtume aliposali akielekea Baytul Maqdis, Mayahudi hukasirika sana na hata husema "inakuaje Mtume wenu anawaamrisheni kutenda kinyume na Mayahudi na inapokuja swala ya ibada basi anauelekea mji wetu (Jerusalem)?" Mtume hakujisikia kabisa vizuri kwa maneno hayo ya Mayahudi na alitamani sana kuelekea Al Kaabah.

Sub-Hanallah! Mara moja Allah Akatelemsha aya inayoelezea: "Tunashuhudia ukiinua uso wako mara kwa mara mbinguni. Basi tutakuelekeza upande wa Qiblah uiridhiayo wewe. Elekea Msikiti wa Haraam (Al Kaaba) sasa hivi, na enyi Waislamu! Elekeze nyuso zenu huko pia, popote mlipo .." (Quran Tukufu 2:144). Zingatieni watukufu Waislamu kuwa badiliko la Qiblah limetokea kwa sababu tu ya kumridhisha Mtume . Kuanzia hapo qiblah yetu ni Al Kaaba huko Makkah.

 

IMAM ABU HANIFA:

 

Jina lake hasa ni Nooman bin Thabit bin Zuta bin Mah. Alizaliwa katika mji wa Kufa, Iraq, mwaka wa 80 Hijria. Alikuwa katika zama tukufu wa Tabi'in (wale waliowafuata Masahaba).

 

Amepokea Abu Huraira RadwiyAllahu Anhu kuwa Mtume amesema kuwa : Katika ummah wangu atakuja mtu ataitwa Abu Hanifa. Siku ya Qiyama yeye (Abu Hanifa) ndiye atakuwa taa ya ummah wangu. Hadithi nyingine imeeleza kuwa "katika kila karne idadi Fulani ya ummah wangu utakuwa na daraja ya juu; Abu Hanifa atakuwa na daraja ya juu zaidi katika zama zake".

 

Miongoni mwa Masahaba aliokutana nao ni Sayyiduna Anas bin Maalik, Sayyiduna Sahl bin Saad na Sayyiduna Abul Tufail Amir bin Wathila RadwiyAllahu Anhum. Imam Abu Hanifa alipata elimu ya dini kupitia baadhi ya Masahaba na wanazuoni wapatao kama 4,000. Baadhi ya Masahaba ni Sayyiduna Hammad Basri, Sayyiduna Ata bin Abi Rabah, Sayyiduna Ikramah, Sayyiduna Imam Baaqir, Sayyiduna Imam Jafar Saadiq, Sayyiduna Abu Ali, Sayyiduna Abu Hurayrah, Sayyiduna Abdullah Ibn Umar, Sayyiduna Aqabah bin Umar, Sayyiduna Safwaan, Sayiduna Jabir na Sayyiduna Abu Qatadah RadwiyAllahu Anhum.

 

Imam Abu Hanifa alikuwa mfanya biashara na kila Ijumaa alikuwa akitoa sarafu 20 za dhahabu kwa wasiojiweza kama sadaka. Kwa muda wa miaka 40 Imam alisali sala ya Alfajiri kwa udhu ule ule wa sala ya Ishai (kwa maana usiku kucha alikuwa katika ibada bila ya kulala). Imam alihiji mara 55. Alihitimisha Quran Tukufu kila siku kimoja na usiku kimoja. Pia alikuwa akihitimisha Quran Tukufu katika rakaa moja ama mbili. Alikuwa mcha Mungu sana kiasi cha kufunga mwaka mzima (isipokuwa siku zile 5 zilizokatazwa) kwa muda wa miaka 30. Mahala alipofariki, alisoma Quran Tukufu 7,000.

WATUKUFU WAISLAMU TUPO JAMANI!!!

Mwezi Sha'abaan mwaka 150 Hijria, Imam aliiaga dunia hii huko Iraq akiwa katika hali ya sala, akiwa na umri wa miaka 70. Jeneza lake lilisaliwa mara 6 na kila mara waumini wapatao 50,000 walihudhuria na wengine walikuja kumuombea kwenye kaburi lake kwa siku karibu 20 hivi.

 

Maswali / maoni yanakaribishwa.

 

JazakAllah.

Jan 25, 2025

Mi-iraj - PT 5 (MWISHO) [Kiswahili]

Assalaamu alaikum,

 

Natumai hamjambo. Namalizia risala yetu kuhusu msafara wa Isra na Mi-'iraj. In sha Allah risala ya mwezi Sha-'abaan itafuata, kwani leo ni mwezi mosi Sha-'abaan. 

 

Baada ya kumshukuru Allah na kumtakia Rahma Mtume Muhammad , hapo juu ni aya ya 8 HADI 10 ya Sura Najmi, inayozungumzia Mtume Muhammad kuonana na Allah.

 

Mtume Muhammad alishuhudia Pepo na moto na baadae kufika Sidrah, ambapo alisikia sauti ya SUB-HANALLAH, ALHAMDULILLAH. Mtume Muhammad aliuliza ni kitu gani hiyo? Jibrail akajibu kuwa Sidrah, ambayo ni mti mkubwa, Malaika huleta dhikri. Hapo ndipo tamati ya Malaika. Mtume Muhammad alimwambia Jibrail waendelee lakini Jabirail akamjibu kuwa akisogea hatua moja kutoka hapa basi mbawa zake zitaungua kutokana na Nuru ya Allah; akamuambia Mtume Muhammad aendelee na safari.

Hapa ndipo Jibrail alimuomba idhini Mtume Muhammad ili amuonyeshe utukufu aliojaaliwa na Allah; kwani siku zote hizo Jibrail alikuwa akimjia Mtume Muhammad katika sura ya binadamu tu. Jibrail alipoondoa pazia mbawa zake 600 zikaonekana na ukubwa wa kila mbawa ulizidi hata ukubwa wa ardhi yote ya dunia. Wanazuoni wanasema lau kama Mtume Muhammad angemuonyesha utukufu wake, basi Jibrail angezimia pengine hadi kiyama.

Baada ya hapo Jibrail alimuomba Mtume Muhammad amtakie idhini kutoka kwa Allah kuwa siku ya kiyama wakati umma wake utakapopita kwenye njia nyepesi, basi yeye atande mbawa zake kuwasalimisha wapite kwa raha.

Baada ya hapo Mtume Muhammad alimpanda Rafraf na kuelekea juu zaidi. Baada ya kupita Arshi ndipo alimuona na Allah kwa macho yake, na hapo ndipo alimkaribia Allah. Kisha Allah Alimjaalia wahyi. Allah Alimuuliza je umeleta nini?

Mtume : Attahiyatu lillahi wasswalawaatu wattayyibaatu.

Allah : Assalaamu alaika ayyuhan Nabiyyu warahmatullahi wabarakaatuhu (salamu ziwe juu yako ewe Mtume pamoja na Rahma na Baraka).

Mtume : Assalaamu alaina wa-alaa ibadillahis swaalihin (salamu ziwe juu yetu na waja wako wema).

Hapo ndipo Allah Alimzawadia sala 50 za kutwa nzima. Mtume Muhammad alianza safari ya kurudi, lakini alipokutana na Mtume Musa katika mbingu ya 6, alimuambia arudi kwa Allah ili zipunguzwe kwani ummah wake walifaradhishiwa sala 2 tu kutwa nzima na walishindwa. Mtume Muhammad alirudi tena kwa Allah kutaka kupunguziwa, na Allah alimpunguzia sala 5. Alipofika tena kwa Mtume Musa, aliambiwa bado ni nyingi na kurudi tena kwa Allah. Kila nenda rudi sala 5 zinapungua hadi kusalia sala 5 na hapo ndipo Mtume Muhammad alisema sasa anaona haya kurudi tena kwa Allah. Ila Allah Alimuambia kuwa ummah wako itasali sala 5 tu lakini Sisi tutamjaalia thawabu za sala 50.

 

Maswali / maoni yanakaribishwa.

 

JazakAllah.

Jan 23, 2025

Mi-iraj - PT 4 [Kiswahili]

Assalaamu alaikum,

 

Natumai hamjambo. Tunaendelea na risala yetu kuhusu msafara wa Isra na Mi-'iraj. 

 

Baada ya Kumshukuru Allah na kumtakia Rehma Mtume Muhammad , hapo juu ni aya ya kwanza ya Sura Bani Israil, ambayo inazungumzia msafara wa miraji.

 

Tafsiri ya aya:

Utukufu ni Wake Yeye Aliyempeleka Mja Wake katika sehemu tu ya usiku kutoka Msikiti wa Haraam (Makkah) hadi Msikiti wa Aqsa (Palestina), ambao umezungukwa na Baraka Zetu, ili Tumuonyeshe baadhi ya alama zetu. Hakika Allah ndiye Mwenye Kusikia Mwenye Kuona.

 

Mtume Muhammad alipoanza safari ya Masjidul Aqsa, njiani alimuona Mtume Musa akisali ndani ya kaburi lake. Hapa tunapata kufahamu kuwa Mitume si tu wapo hai ndani ya makaburi yao, bali huwa wanasali na pia hupata rizki.

 

Mtume Muhammad alipofika Masjidul Aqsa, Jibrail alitoboa sehemu moja iitwao Sakhra na kisha kumfunga mnyama wao. Kisha Jibrail alitoa adhana juu ya Msikiti wa Sakhra na kurudi Masjidul Aqsa. Hapa Mitume wote walikuwepo na kila mmoja akawa anafikiria je ni Mtume Adam ambae ni baba wa binadamu wote, ndiye atakaesalisha leo? Au Khalili wa Allah, Mtume Ibrahim? Au ni Mtume Nuh kwani baada ya tufani ya zama zake, masuala ya uzaaji ulianza kupitia yeye. Lakini Jibrail alimshika mkono Mtume Muhammad na kumpeleka mbele na kumuambia awa imamu wa Mitume wote. Baada ya sala, kila Mtume alisoma khutba ya kumsifu Mtume Muhammad .

 

Baada ya hapo Mtume Muhammad alifuatana na Jibrail kuelekea mbinguni. Kuna riwaya 2; (1) walienda kumtumia mnyama yule yule Buraaq au (2) Miraji ni jina la ngazi mmoja na hivyo walitumia ngazi hiyo kuelekea juu. Walipofika mbingu ya 1, mlango ulikuwa umefungwa. Jibrail alipiga hodi na kuulizwa ni nani? Alijibu mimi Jibrail niko na Mtume Muhammad . Baada ya kuulizwa kama Mtume Muhammad ameitwa, Jibrail akajibu kuwa ndiyo.

 

Mtume Muhammad alimuona mzee mmoja ambae kila akiangalia vivuli upande wake wa kulia basi hutabasamu lakini anapoangalia vivuli upande wa kushoto basi hulia. Mtume Muhammad aliuliza ni nani huyo na kwa nini mara hutabasamu na mara hulia? Jibrail alijibu kuwa msalimie huyu ni mtume Adam, upande wake wa kulia ni watoto wake walioleta imani na ndyo maana hutabasamu akiwaona. Wale wa kushoto ni watoto wake waliokataa imani na ndyo maana hulia akiwaona.

 

Mtume Muhammad alianza kuchupa mbingu moja baada ya nyingine huku akikutana na Mitume kila mbingu. Mbingu wa 2 alikutana na Mtume Yahya na isa, ya 3 Mtume Yusuf, ya 4 Mtume Idris, ya 5 Mtume Harun, ya 6 Mtume Musa nay a 7 alikutana na Mtume Ibrahim aliekaa kwa kuegemea Baitul Maamur. Baitul Maamur ni kibla ya Malaika mbingu ya 7, ambamo kila asubuhi na jioni Malaika 70,000 wapya huingia hapo. Mtume Muhammad aliwasalisha Malaika.

 

Maswali / maoni yanakaribishwa.

 

JazakAllah.

Jan 22, 2025

Mi-iraj - PT 3 [Kiswahili]

Assalaamu alaikum,

Natumai hamjambo. Leo ni usiku wa Isra wal Mi-'iraj.

Picha hapo chini ni sehemu takatifu mno ndani ya Masjidul Aqsa, nchini Palistina, ambapo Mtume alianza safari yake hapo ya kwenda mbinguni. Jiwe hilo linaitwa SAKHRAA.

Jan 21, 2025

Mi-iraj - PT 2 [Kiswahili]

Assalaamu alaikum,

 

Natumai hamjambo. Tunaendelea na risala yetu kuhusu msafara wa Isra na Mi-'iraj. Ijumaa Kareem

 

 

Kwanza kabisa hebu iangalie kwa makini jiwe katika picha niliyoambatanisha. Usiku wa Mi-'iraj wakati Mtume alipoanza safari ya kupaa mbinguni pamoja na mnyama Burraq, hilo jiwe nalo likaanza kupaa. Hapo ndipo Mtume alipoiamuru kusimama, na kwa kuwa ilikuwa imeshaanza kupaa basi jiwe ikasimama hivyo hivyo hewani na hadi leo hii jiwe hilo lipo kando kidogo na Masjidul Aqsa, Palestina.

 

 

 

 

 

Baada ya Kumshukuru Allah na kumtakia Rehma Mtume Muhammad , hapo juu ni aya ya kwanza ya Sura Bani Israil, ambayo inazungumzia msafara wa miraji.

 

Tafsiri ya aya:

Utukufu ni Wake Yeye Aliyempeleka Mja Wake katika sehemu tu ya usiku kutoka Msikiti wa Haraam (Makkah) hadi Msikiti wa Aqsa (Palestina), ambao umezungukwa na Baraka Zetu, ili Tumuonyeshe baadhi ya alama zetu. Hakika Allah ndiye Mwenye Kusikia Mwenye Kuona.

 

Imeelezwa kwenye vitabu vya Bukhari na Muslim kuhusiana na msafara huo kuwa Mtume Muhammad alikuwa nyumbani kwa Ummi Haani, kisha aliletwa sehemu inaitwa Hatim ndani ya Msikiti Mtukufu wa Makkah. Hapa alipasuliwa kifua, moyo ulitolewa na kuoshwa na maji matukufu ya zamzam na kujazwa hikma ndani yake na kisha kurudishwa na baada ya hapo kifua kikashonwa. Baada ya hapo Malaika mtukufu Jibrail Alaihissalaam alimuambia kuwa Allah Amemuita. Aliletwa mnyama mmoja aitwae Burraaq, ambae ni mkumbwa kuliko punda na mdogo kuliko farasi, aliye na kasi kiasi cha kuwa hatua yake moja umbali wake ni sawa na tamati ya sisi kuona. Mtume Muhammad alimpanda na kuanza safari ya kwenda Msikiti wa Aqsa.

 

Mtume Muhammad alionyeshwa baadhi ya alama wakati anaelekea Msikiti wa Aqsa, nazo ni kama ifuatavyo:

 

1. Mtume Muhammad aliwaona baadhi ya watu wakilima, huku wanaendelea kupanda mbegu na papo hapo mazao yalikamilika na watu hao kuvuna na kupata faida. Mtume Muhammad alifahamu kila kitu, lakini kuuliza kwake ni kwa ajili ya mafundisho kwetu.

Aliuliza: hivi ni kina nani hao?

Jibrail alimjibu: hawa ni katika ummah wako wanaotoa katika njia ya Allah; mfano kujenga Misikiti, madrasa, nk basi hupata faida papo hapo tu.

 

2. Mtume Muhammad aliwaona watu wamelala na vichwa vyao kupondwa, kisha husima wakiwa wazima na baadae hulala na vichwa hupondwa.

Aliuliza: ni kina nani hao:

Jibrail almijibu: hao ni wale wanaopendelea kulala wakati wa sala ya Alfajiri, wanaona usingizi mtamu na pia huacha sala. Wataadhibiwa hivyo hadi siku ya Kiyama.

 

3. Mtume Muhammad aliwaona baadhi ya watu wakila mawe na miti porini lakini hawashibi.

Aliuliza: ni kina nani hao?

Jibrail alimjibu: hao ni wale wasiotoa zaka kutokana na walichojaaliwa na Allah na pia hula haki za masikini.

Mtume Muhammad amesema kuwa toeni zaka ili mkinge mali zenu.

 

4. Mtume Muhammad aliwaona watu ambao wamewekewa vyakula mbalimbali halali na vizuri sana mbele yao, lakini wanayaacha hayo na kukimbilia kula vyakula vibaya vilivyooza na kutoa herufu mbaya.

Aliuliza: ni kina nani hao?

Jibrail alimjibu: hao ni wale wanaowaacha wake zao halali na hukimbilia kwa wanawake wa nje na kutenda mambo ya haramu.

 

5. Mtume Muhammad alimuona mtu mmoja mwembamba sana aliyekusanya kuni nyingi. Alipotaka kuubeba akashindwa. Badala ya kupunguza kuni kidogo, akaenda porini kuongeza kuni zingine.

Aliuliza: ni nani huyo?

Jibrail alimjibu: ni yule mwenye kuleta khiyana kwenye amana za watu na pia huweka tamaa apewe amana zaidi.

 

6. Mtume Muhammad aliwaona baadhi ya watu wakikata taya zao kwa kisu kikali. Wanapomaliza za upande wa kulia na kukata za upande wa kushoto, za kulia huwa sawa.

Aliuliza: ni kina nani hao?

Jibrail alimjibu: hao ni wale wanaoeneza fitina kwa ulimi wao.

 

Hizo ni baadhi alama alizoonyeshwa Mtume Muhammad katika msafara wake.

 

Maswali / maoni yanakaribishwa.

 

JazakAllah.

Jan 20, 2025

Mi-iraj - PT 1

Assalaamu alaikum,

 

Natumai hamjambo. Kama mnavyofahamu kuwa mwezi tulionao ni wa Rajab na usiku wa Jumatatu (24/4/2017) kuamkia Jumanne (25/4/2017) ni katika usiku takatifu katika historia ya Kiislam, kwani ni usiku ambamo Mtume wetu mpendwa alijaaliwa muujiza wa isra na Mi-'iraj.

Hivyo nitakuwa natuma risala fupi fupi kuhusu msafara huo in sha Allah.

 

 

 

 

Baada ya Kumshukuru Allah na kumtakia Rehma Mtume Muhammad Swall-Allahu Alaihi Wasallam, hapo juu ni aya ya kwanza ya Sura Bani Israil, ambayo inazungumzia msafara wa miraji.

 

Ieleweke kuwa kila Mtume aliyeletwa hapa duniani alipewa muujiza au miujiza.

Lakini Mtume Muhammad Swall-Allahu Alaihi Wasallam aliletwa kama muujiza licha ya kupewa miujiza mingi, mmojawapo ukiwa huu msafara wa miraji.

 

Tafsiri ya aya:

Utukufu ni Wake Yeye Aliyempeleka Mja Wake katika sehemu tu ya usiku kutoka Msikiti wa Haraam (Makkah) hadi Msikiti wa Aqsa (Palestina), ambao umezungukwa na Baraka Zetu, ili Tumuonyeshe baadhi ya alama zetu. Hakika Allah ndiye Mwenye Kusikia Mwenye Kuona.

 

Tukiichunguza aya peke yake tu ina nukta nyingi za kuzingatia.

1. Kwanza kabisa, Allah Ametaja Utukufu Wake kwa kuanza aya. Hii ni kuukata kata kabisa utata uliotokea na utakaotokea kwani mwenye kuleta utata katika msafara huu, basi moja kwa moja analeta mashaka katika uwezo wa Sub-hana!

2. Baadhi ya watu wanadai kuwa eti Mtume Swall-Allahu Alaihi Wasallam alioteshwa tu kwenda mbinguni na si kuwa alienda (yaani eti mwili wake haukuenda)!!! Sehemu ya pili ya aya inafafanua : "ALIYEMPELEKA MJA WAKE". Sehemu ya aya haisemi kuwa "alimuotesha"! Hivyo mwenye kupinga msafara huo wa kiwiliwili na roho basi atatoka katika Uislamu.

3. Msafara huu ulifanyika katika sehemu fupi mno ya usiku. Riwaya moja inaelezea ufupi wa msafara kuwa maji aliyotawadhia Mtume Swall-Allahu Alaihi Wasallam yalikuwa bado yanasambaa ardhini wakati Mtume Swall-Allahu Alaihi Wasallam aliporejea. Riwaya nyingine inasema kuwa Mtume Swall-Allahu Alaihi Wasallam alipofungua mlango kutoka chumbani mwake, ile komeo (cheni) bado ilikuwa ikicheza aliporejea! Kwa ufupi hatuwezi kupata picha ya ufupi wa msafara huo na ndiyo maana ikatajwa kuwa ni muujiza.

4. Vile vile ni sababu ya msafara kuwa usiku tu? Sababu kuwa iliyotajwa kuwa ili watu wasipate kuona. Imani ni kuamini kisichoonekana, hivyo lau kama msafara ungetokea mchana basi wengi wangemuona Mtume Swall-Allahu Alaihi Wasallam akienda na hivyo kupima imani ingekuwa ngumu.

5. Kwa nini sehemu ya kwanza ya msafara ulikuwa kutoka Makkah hadi Palestina? Hii ni kwa sababu Waarabu walikuwa na misafara ya mara kwa mara baina ya sehemu hizo. Hivyo kuwafahamisha kuwa msafara huu wa Mtume Swall-Allahu Alaihi Wasallam baina ya sehemu hizo katika muda mfupi ili wawe na picha ya sehemu wanazoambiwa.

 

Maswali / maoni yanakaribishwa.

 

JazakAllah.

Jan 5, 2025

RAJAB-UL-MURAJJAB - PT 4 [Kiswahili]

Assalaamu alaikum,

 

Natumai hamjambo. Mwezi 6 Rajab mmoja katika kiongozi wa masharifu kwa tarika ya Chishti aliiaga dunia na ifuatayo ni risala fupi.

 

 

SULTAN MUINUDDIN CHISHTI RAHIMAHULLAH.

 

Sultan Muinuddin Chishti Rahimahullah alizaliwa Khorasan, Afghanistan. Alikuwa mwaka sambamba na Sayyid AbdulQadir Jilani Qaddasallahu Sirrah. Kwa kuwa Sayyid AbdulQadir Jilani Qaddasallahu Sirrah alishachaguliwa kuiongoza bara la Uarabuni kuhuisha dini, Mtume alimchagua Sultan Muinuddin Chishti Rahimahullah kuiongoza bara Hindi katika kuinusuru dini. Hakuwahi kupita maeneo ya bara Hindi wala hakufahamu kabisa lugha ya kihindi. Mtume alimjia kwenye ndoto na kumuonyesha njia ya kwenda bara Hindi na kisha alimtemea mate matukufu na hivyo akafahamu lugha ya kihindi kwa fasaha.

 

Kutokana na karama zake, wachawi wa kibaniani wakajua huo ni uchawi, hivyo mfalme wa huko aliwakusanya wachawi wakubwa kukabiliana nae lakini wote walishindwa na hatimaye kusilimu. Zaidi ya mabaniani milioni 9 walisilimu kutokana na karama zake tofauti. Hatimaye aliiaga dunia mwezi 6 Rajab.

 

Maswali / maoni yanakaribishwa

 

JazakAllah.

Jan 3, 2025

RAJAB-UL-MURAJJAB - PT 3 [Kiswahili]

Assalaamu alaikum,

 

Natumai hamjambo. Mwezi 4 Rajab ambamo mmoja katika maimamu wetu wane, Imam Shafi-'I aliiaga dunia.

 

 

Baada ya kumshukuru Allah na kumtakia Rahma Mtume Muhammad , aya hapo juu ya 36 ya Sura Tawbah, inazungumzia utukufu wa miezi minne. Mwezi Rajab, ambao ni mmojawapo kati ya miezi hiyo minne, mwezi ambao una fadhila tele. Ni mwezi ambamo dua hukubalika.

TAFSIRI: Bila shaka idadi ya miezi kwa Allah ni miezi kumi na mbili katika kitabu cha Allah tangu Alipoumba mbingu na ardhi, miongoni mwao minne ni yenye huruma (tukufu). Hii ni dini iliyonyooka na hivyo msidhulumu nafsi zenu katika miezi hizo. Na piganeni na washirikina wote kama wao wanavyopigana nanyi nyote, na jueni kuwa Allah yu pamoja na wachamungu.

 

IMAM SHAFI-'I RAHIMAHULLAH.

Jina la Imam Shafi-'I ni Muhammad bin Idris bin Abbas bin Uthman bin Shafi-'I bin Saib bin Ubeid bin Abdi Yazid bin Hashim bin Abdul Muttalib bin Abdi Manaf.

 

Abdi Manaf ni katika ukoo wa nne wa Mababu zake Mtume . Ukoo wa Mtume Swall-Allahu Alaihi Wasallam uko hivi: (Sayyidina) Muhammad bin Abdullah bin Abdul Muttalib bin Hashim bin Abdi Manaf. Hivyo Mtume amezaliwa kupitia mwanae Abdi Manaf (Hashim) wakati Imam Shafi-'I amezaliwa kupitia Abdul Muttalib.

Imam Shafi-'I amekuwa maarufu kwa jina hilo (Shafi-'i)  kupitia kwa babu yake katika ukoo wa tatu (Shafi-'i).

 

Wazazi wake wanatokana na kabila maarufu la kiarabu la Bani Hashim. Baadhi ya sababu ya yeye kuwa na kipaji hicho ni kuwa alikuwa : Imam (kiongozi – wa Dini), Mwanasheria (wa masuala ya sharia za Dini), Mcha Mungu na mtu mwenye hekima na busara. Alikuwa mwandishi wa vitabu vikubwa 14 vya kanuni na falsafa vya sharia ya Kiislam na pia vitabu vingine vidogo zaidi ya 100.

 

Kila alipopatwa na tatizo, Imam Shaifi-'I alielekea Baghdad kudhuru kaburi la Imam Abu Hanifa, kisha husali rakaa 2 na kumuomba Allah kupitia (wasila) kwa Imam Abu Hanifa. Imam Shafi-'I mwenyewe amesema kuwa hakika maombi yanakubalika katika kaburi la Imam Abu Hanifa.

 

Imam Shafi-'I alikuwa mwanafunzi wa Imam Malik Radwiy-Allahu Anhu. Alikuwa akihitimisha Quran (Msahafu) nzima katika usiki moja tu mwezi Ramadhani. Alihifadhi Qurani nzima akiwa na umri wa miaka 7 tu.

 

Alizaliwa mwaka 150 Hijriya (mwaka ambamo Imam Abu Hanifa aliiaga dunia), huko Asqalan au Mina au Ghizza. Aliishi Makkah na aliiaga dunia hii akiwa na umri wa miaka 53, mwaka 204 Hijriya huko Misri.

 

Maswali / maoni yanakaribishwa

 

JazakAllah.

Jan 1, 2025

RAJAB-UL-MURAJJAB - PT 2 [Kiswahili]

Assalaamu alaikum,

 

Natumai hamjambo. Mwezi wa Rajab tumeshauanza na ifuatayo ni sehemu ya kwanza ya risala …

 

 

Baada ya kumshukuru Allah na kumtakia Rahma Mtume Muhammad , aya hapo juu ya 36 ya Sura Tawbah, inazungumzia utukufu wa miezi minne. Mwezi Rajab, ambao ni mmojawapo kati ya miezi hiyo minne, mwezi ambao una fadhila tele. Ni mwezi ambamo dua hukubalika.

TAFSIRI: Bila shaka idadi ya miezi kwa Allah ni miezi kumi na mbili katika kitabu cha Allah tangu Alipoumba mbingu na ardhi, miongoni mwao minne ni yenye huruma (tukufu). Hii ni dini iliyonyooka na hivyo msidhulumu nafsi zenu katika miezi hizo. Na piganeni na washirikina wote kama wao wanavyopigana nanyi nyote, na jueni kuwa Allah yu pamoja na wachamungu.

                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                   

Mwezi wa saba katika kalenda ya Kiislam inaitwa RAJAB, ambayo inatokana na neno "TARJIB", yenye maana ya heshima na hata zama za ujahili Waarabu waliuheshimu sana mwezi huu kwa kuacha mapigano na mauaji, wakisema ni mwezi wa Mwenyezi Mungu.

Mtume amesema kuwa Rajab ni mwezi wa Allah, Shaaban ni wa kwangu na Ramadhani ni ya ummah wangu.

 

Mtume amesema kuwa Rajab ni mwezi wenye fadhila nyingi, thawabu ya amali njema huwa maradufu ya thawabu ya kawaida. Mwenye kufunga swaum 1 ndani ya Rajab, basi ni sawa na kufunga mwaka mzima.

Siku 1 Mtume Isa Alaihissalaam alipokuwa akipita karibu na mlima mmoja, aliona nuru sehemu Fulani ya mlima. Alimuomba idhini Allah ili aweze kuzungumza na mlima. Mlima ilimuuliza nini atakacho?  Mlima ikasema kuwa ndani yake kuna Mcha Mungu mmoja nan i kwa sababu ya huyo mlima una nuru. Mtume Isa Alaihissalaam alimuomba Allah aonyeshwe huyo mtu na mara mlima ikapasuka na akaonekana Mcha Mungu aliye mzuri sana. Alisema kuwa yeye ni katika watu wa Mtume Musa Alaihissalaam na alimuomba Allah Amjaalie maisha marefu ili aweze kushuhudia zama za Mtume wa mwisho Muhammad na hivyo ahesabiwe miongoni mwa ummah wa Mtume wa mwisho. Mcha Mungu huyo alikuwa mlamani humo kwa miaka 600. Kisha Mtume Isa alimuuliza Allah kama kuna Mcha Mungu ardhini zaidi ya huyo bwana? Allah alimjibu: "Ewe Isa, lau kama mja wangu katika ummah wa Mtume wa mwisho akifunga siku moja tu ya mwezi Rajab, basi huyo mja kwangu atakuwa Mcha Mungu zaidi kuliko huyo bwana!! (SUB-HANALLAH).

 

Baadhi ya tarehe muhimu:

Tarehe 1 – Mtume Nuh Alaihissalaam alianza safari na wafuasi wake katika mashua (meli) waliyoitengeneza.

Tarehe 4 – Vita vya Safin

Tarehe 4 – Imam Shafi-I Rahmatullahi Alaihi kuiaga dunia

Tarehe 6 – Sayyidina Moinuddin Chishti (kiongozi wa Walii kwa twariqa ya Chishtiya) kuiaga dunia

Tarehe 27 – Msafara wa isra na Mi-iraj ya Mtume .

 

 

 

Tarehe 1 Mtume Nuh na wafuasi wake walianza safari katika meli kabla ya tufani kali iliyowaangamiza waliompinga.

 

 

Tarehe 4: Imam Shafi aliaga dunia. Jina lake ni Muhammad bin Idris na kizazi chake cha 4 kinakutana na kile cha Mtume Muhammad kwa Abdi Manaf. Amezaliwa mwaka 150 hijria na kufariki mwaka 204h mjini Cairo, Misri. Alikuwa akikhitimisha msahafu mmoja kila siku katika mwezi Ramadhani. Kila alipopatwa tatizo, basi huenda kuizuru kaburi la Imam Abu Hanifa na kisha huomba dua akimtawassul.

 

 

 

Tarehe 6: Walii mkubwa wa Allah Moinuddin Chishti aliaga dunia nchini India. Walii huyo alikuwa mwaka sambamba na Sheikh Abdul Qadir Jilani Qaddasallahu Sirrah. Mtume Muhammad alimjaalia uwalii wa bara hindi. Mabaniani milioni 9 walisilimu kwa jitihada zake.

 

 

Tarehe 27: Msafara wa Isra na miraj ya Mtume Muhammad ambayo insha Allah tutaanza kuizungumzia hapo baadae.

 

Maswali / maoni yanakaribishwa

 

JazakAllah.

 

Visitor's Traces

1,277 Pageviews
Mar. 06th - Apr. 06th

Total Page views

763804