Ads 468x60px

Feb 28, 2014

Shaikh AbdulQadir Jilani - PT 3‏ (Kiswahili)


Assalaamu alaikum,
Natumai hamjambo.  Ijumaa Kareem
Namalizia risala fupi kuhusu kiongozi wa Mawalii (Masharifu) – Shaikh Sayyid AbdulQadir Jilani RadwiyAllahu Anhu.

AYA:  ALAA INNA AWLIYA ALLAHI LA KHAUFUN ALAIHI WALAHUM YAHZANUN. (YUNUS: 62)
Baada ya kumshukuru Allah na kumtakia Rahma Mtume Muhammad Swallallahu Alaihi wasallam, imesomwa aya ya Sura Yunus, inayozungumzia mawalii wa Allah na ndiyo itakuwa mada yetu leo kwani huu ni Mfungo 7 au Rabi ul Akhar, ambamo kiongozi wa Mawalii, Sheikh AbdulQadir Jilani aliiaga dunia.
AYA: Jihadharini, marafiki wa Allah hawana hofu wala huzuni.

Sheikh alikuwa mkarimu sana na hivyo aliwasaidia sana wanafunzi wenzake wenye hali duni. Kwa kuwa umasikini ulienea zama hizo, na baada ya Sheikh kumaliza pesa zake, alikuwa akienda porini kula aidha majani au mizizi ya baadhi ya mimea yenye kutoa maji. Sheikh alikaa siku kadhaa katika ibada ya Allah bila ya kula wala kunywa, kisha husikia sauti (ya Allah) ikimwambia “ewe AbdulQadir kunywa” na “ewe AbdulQadir kula”, ndipo hula na kunywa.
Kuna karama nyingi zilizodhihirika kupitia kwa Sheikh, mmojawapo ikiwa kuhudhuria sehemu 70 za mwaliko kwa wakati mmoja tu!! Vile vile mawaidha yake yalihudhuriwa na watu wapatao 70,000 kwa wakati mmoja. Enzi hizo hapakuwepo na vipaza sauti na hivyo desturi ilikuwa hivi; mmojawapo katika waliohudhuria husimama pale ambapo sauti humfikia na kisha huwasimulia wenzake walio nyuma. Lakini karama nyingine ya Sheikh ni kuwa Yule aliyekaa mwisho husikia kama anavyosikia aliyekaa mbele ya Sheikh! Allah amemuahidi Sheikh kuwa mfuasi wake hatakufa hadi ajaaliwe toba.
Habari za Sheikh ni nyingi mno na kwa nini isiwe hivyo kwani yeye ndiye kiongozi wa Mawalii wote wa Allah. Pia ikumbukwe kuwa karama za Mawalii (hata za umma zilizopita) zimo ndani ya Quran Tukufu. Pia ieleweke kuwa jambo lolote ambalo akili haikubaliani nalo, linapotendwa na Mitume basi huitwa MUUJIZA, na jambo la namna hiyo inapotendwa na Masahaba au Mawalii basi huitwa KARAMA.
Maswali / maoni yanakaribishwa.
JazakAllah,
Muhammad KHATRI 

0 comments:

Post a Comment

Enter your Comment here...

 

Visitor's Traces

Total Page views