Ads 468x60px

Jun 4, 2013

ISRA NA MI-'IRAJ - PT 3‏ (Kiswahili)

Assalaamu alaikum,
Natumai hamjambo. Natumai mnakumbuka tulipoishia katika risala yetu ya Mi-‘iraj. Mtume Swallallahu Alaihi Wasallam alianza safari yake kuelekea Msikiti wa Aqsa na njiani alionyeshwa baadhi ya alama.
SUB-HANALLADHI ASRA BI-ABDIHI LAYLAN MINAL MASJIDIL HARAAMI ILAL MASJIDIL AQSA, ALLADHI BAARAKNA HAWLAHU LINURIYAHU MIN AYATINA, INNAHU HUWAS SAMIUL BASIR. (SURA BANI ISRAIL, AYA 1)
Baada ya Kumshukuru Allah na kumtakia Rehma Mtume Muhammad Swallallahu Alaihi Wasallam, aya hapo juu ni ya kwanza ya Sura Bani Israil, ambayo inazungumzia msafara wa miraji.
Tafsiri ya aya:
Utukufu ni Wake Yeye Aliyempeleka Mja Wake katika sehemu tu ya usiku kutoka Msikiti wa Haraam (Makkah) hadi Msikiti wa Aqsa (Palestina), ambao umezungukwa na Baraka Zetu, ili Tumuonyeshe baadhi ya alama zetu. Hakika Allah ndiye Mwenye Kusikia Mwenye Kuona.
Mtume Muhammad Swallallahu Alaihi Wasallam alipokuwa akielekea Masjidul Aqsa, njiani alimuona Mtume Musa akisali ndani ya kaburi lake. Hapa tunapata kufahamu kuwa Mitume si tu wapo hai ndani ya makaburi yao, huwa wanasali na pia hupata rizki.
Mtume Muhammad Swallallahu Alaihi Wasallam alipofika Masjidul Aqsa, Jibrail alitoboa sehemu moja iitwao Sakhra na kisha kumfunga mnyama wao. Kisha Jibrail alitoa adhana juu ya Msikiti wa Sakhra na kurudi Masjidul Aqsa. Hapa Mitume wote walikuwepo na kila mmoja akawa anafikiria je ni Mtume Adam ambae ni baba wa binadamu wote, ndiye atakaesalisha leo? Au Khalili wa Allah, Mtume Ibrahim? Au ni Mtume Nuh kwani baada ya tufani ya zama zake, masuala ya uzaaji ulianza kupitia yeye. Lakini Jibrail alimshika mkono Mtume Muhammad Swallallahu Alaihi Wasallam na kumpeleka mbele na kumuambia awa imamu wa Mitume wote. Baada ya sala, kila Mtume alisoma khutba ya kumsifu Mtume Muhammad Swallallahu Alaihi Wasallam.

Baada ya hapo Mtume Muhammad Swallallahu Alaihi Wasallam alifuatana na Jibrail kuelekea mbinguni. Kuna riwaya 2; (1) walienda kumtumia mnyama yule yule Buraaq au (2) Miraji ni jina la ngazi mmoja na hivyo walitumia ngazi hiyo kuelekea juu. Walipofika mbingu ya 1, mlango ulikuwa umefungwa. Jibrail alipiga hodi na kuulizwa ni nani? Alijibu mimi Jibrail niko na Mtume Muhammad Swallallahu Alaihi Wasallam. Baada ya kuulizwa kama Mtume Muhammad Swallallahu Alaihi Wasallam ameitwa, Jibrail akajibu kuwa ndiyo.

Mtume Muhammad Swallallahu Alaihi Wasallam alimuona mzee mmoja ambae kila akiangalia vivuli upande wake wa kulia basi hutabasamu lakini anapoangalia vivuli upande wa kushoto basi hulia. Mtume Muhammad Swallallahu Alaihi Wasallam aliuliza ni nani huyo na kwa nini mara hutabasamu na mara hulia? Jibrail alijibu kuwa msalimie huyu ni mtume Adam, upande wake wa kulia ni watoto wake walioleta imani na ndyo maana hutabasamu akiwaona. Wale wa kushoto ni watoto wake waliokataa imani na ndyo maana hulia akiwaona.

Mtume Muhammad Swallallahu Alaihi Wasallam alianza kuchupa mbingu moja baada ya nyingine huku akikutana na Mitume kila mbingu. Mbingu wa 2 alikutana na Mtume Yahya na isa, ya 3 Mtume Yusuf, ya 4 Mtume Idris, ya 5 Mtume Harun, ya 6 Mtume Musa nay a 7 alikutana na Mtume Ibrahim aliekaa kwa kuegemea Baitul Maamur. Baitul Maamur ni kibla ya Malaika mbingu ya 7, ambamo kila asubuhi na jioni Malaika 70,000 wapya huingia hapo. Mtume Muhammad Swallallahu Alaihi Wasallam aliwasalisha Malaika.

FAIDA YA QURAN:-
1.       Surah Al Fatihah ina nguvu ya uponyaji wa magonjwa yote. Soma Surah Al Fatihah kabla ya kuanza kazi yoyote muhimu maishani.

2.       Iwapo utasoma aya 4 za Surah Al Baqarah ikifuatiwa na Ayatul Kursi na aya 3 za Surah hii, shetani atakaa mbali.


Maoni / maswali yanakaribishwa.
JazakAllah,
Muhammad KHATRI



0 comments:

Post a Comment

Enter your Comment here...

 

Visitor's Traces

Total Page views